Mahakama ya Kenya imesitisha utekelezaji wa makubaliano ya msaada wa afya yenye thamani ya $2.5bn (£1.9bn) yaliyosainiwa na Marekani wiki iliyopita kutokana na wasiwasi kuhusu faragha ya data. Hatua hiyo inafuatia kesi iliyowasilishwa na shirika la kutetea haki za watumiaji likitaka kusitishwa kwa kile linachodai kuwa ni uhamishaji na ushirikishwaji wa data binafsi za Wakenya chini ya makubaliano hayo. Uamuzi ...

















