Matokeo ya awali ya uchaguzi Uganda 2026, yalitolewa muda mfupi kabla ya saa tano usiku yanaonyesha Rais Yoweri Museveni wa NRM aliyemadarakani anaongoza kwa asilimia zaidi ya 60 ya kura zilizopigwa.
Jaji Simon Byabakama, mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Uganda alisema matokeo hayo yamezingatia vituo 133 vya kupiga kura yaliowakilisha asilimia 0.26 ya jumla ya kura zilizopigwa.
Byabakama alithibitisha kuwa taarifa zingine juu ya uchaguzi zitatolewa Ijumaa, saa tatu asubuhi wakati matokeo zaidi yanaendelea kuwasilishwa katika kituo kikuu cha kuhesabu kura kilichoko eneo la Wakiso.
Awali, Jaji Byabakama alisema kuwa siku ya uchaguzi ilikwenda vizuri ingawa uchaguzi huo ulikumbwa na changamoto za hitilafu ya kimitambo ikiwa ni pamoja na mashine za kupiga kura zilizoshindwa kufanyakazi na kulazimisha shughuli ya upigaji kura kuendelea kwa njia ya kawaida.
Matokeo rasmi ya uchaguzi huu huo yanatarajiwa kutolewa ndani ya saa 48 baada ya zoezi la upigaji kura kukamilika.





Leave a Reply
View Comments