JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA
OFISI YA WAZIRI MKUU
KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU
TAARIFA KWA UMMA
TANGAZO LA FURSA 800 ZA AJIRA YA UDEREVA NCHINI QATAR
Ofisi ya Waziri Mkuu – Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu kwa Kushirikiana na kampuni tanzu ya Mkapa Foundation Imara Horizon, “Connect General Supplies Co. Ltd”, “Sassy Solutions Co. Ltd” pamoja na “Larali Global Solutions” inawatangazia Watanzania wenye sifa kutuma maombi kwa ajili ya kujaza nafasi 800 za fursa za udereva zilizotangazwa na kampuni ya MOWASALAT ya nchini Qatar kama ilivyoelezwa katika jedwali hapa chini: –
MAELEZO YA FURSA
-
Fursa: Dereva
-
Kampuni: Mowasalat
-
Nchi: Qatar
-
Umri: Miaka 25 – 45
Sifa Mwombaji:
-
Awe na elimu ya kidato cha Nne na kuendelea;
-
Awe na uzoefu wa zaidi ya miaka 2 katika fani ya Udereva;
-
Awe na uwezo wa kuzungumza lugha ya Kiingereza;
-
Mwenye uelewa na lugha ya Kiarabu atapewa kipaumbele.
Mambo muhimu
-
Mshahara utalipwa kulingana na Sera ya kampuni pamoja na sheria za nchi ya Qatar;
-
Gharama za matibabu kwa kipindi chote cha ajira zitakuwa juu ya muajiri;
-
Mwajiri atagharamia visa na tiketi ya ndege;
-
Mwajiri atagharamia malazi na chakula katika kipindi chote cha ajira;
Aina ya Ajira: Mkataba
Daraja la Leseni: Daraja C au E
Mwisho wa Kupokea maombi: 16 Mei, 2025
Jinsi ya kutuma maombi
-
https://mkapafoundation.or.tz/index.php/international-career/
-
Simu Na. +255749639354, +255678203223
-
-
https://www.manpower.cgs.co.tz
-
Simu Na. +255748882255, +255675899410
-
-
Sasysolution@gmail.com
-
Simu Na +255782821089 / +255710882820
-
-
-
Simu Na. +255694521912
-
Baada ya kutuma maombi unapaswa kujisajili https://jobs.kazi.go.tz
Simu Na. +255784301987
Tangazo hili limetolewa na:
KITENGO CHA MAWASILIANO SERIKALINI
OFISI YA WAZIRI MKUU
KAZI, VIJANA, AJIRA NA WENYE ULEMAVU
Leave a Reply
View Comments